June 16, 2025 07:54:56 AM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Kaka wa Askofu wa kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima aitwaye Methusela Gwajima amemtaka mdogo wake kwenda kumuomba radhi Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki Dar es Salaam Mhadhama Polycarp Kadinali Pengo kwa kutoa lugha ya kumkashifu.

Akizungumza na wanahabari leo Jijini Dar es Salaam, Methusela alisema ameamua kutokufumbia macho kitendo cha ndugu yake kumkashifu Pengo na kwamba anapaswa kujitathimini alipopotoka kwa kumtukana kiongozi mkubwa wa kiroho kwani ni sawa na kuidhalilisha familia nzima ya Ukoo wa Gwajima.

Alisema maneno yake ya kashfa ni dhahili ya kuwa hata ukoo mzima umedhalilishwa hivyo familia ya Methusela Gwajima  imemtaka  kuomba radhi mara moja.

Hata hivyo alisema kuwa yeye ni kada wa CCM hivyo amepata usumbufu mkubwa tokea sakata hilo liibuke maana ndugu na marafiki walioko nje ya nchi wamekuwa wakimuuliza kuhusiana na suala hilo hali inayompa wakati mgumu kuwapatia majibu.

Alisema kashfa hizo hazina tija kwa taifa na haileti uhusiano mwema baina ya madhehebu ya dini, bali  yanachochea  chuki, uhasama, utengano na hasira kati ya wakristo kwa wakristo.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
31 Mar 2015

Post a Comment

 
Top