April 2, 2025 09:11:16 AM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mke wa mwanamuzik Noorah, Camila Kingwalu amefariki dunia jana nyumbani kwao Morogoro baada ya kuugua kwa muda mrefu.
11008208_1566860043566743_2093446419_n
Akizungumza na Bongo5, ndugu wa karibu wa marehemu ambaye hakutaka kutajwa jina lake, amesema Camila baada ya kuanza kuugua alirudi nyumbani kwao mpaka mauti yalipomkuta hapo jana.
“Kweli amefariki alikuwa kwao Morogoro na bado haikujulikana alikuwa anaumwa nini na mume wake naye anaumwa yupo kwao Shinyanga,” amesema.
20150303014602

Marehemu Camila

“Kwahiyo msiba upo Morogoro, kuna mtu ambaye anaelekea Morogoro sasa hivi akifika kule tutajua kila kitu. Morogoro alienda muda kidogo baada ya kuachana na mume wake. Baada ya kuachana, Noorah akaenda kwao na mke wake akaenda kwao. Hawakubahatika kuwa na watoto,” ameongeza.
“Marehemu alikuwa anaitwa Anna Kigwalu lakini baada ya kuolewa na Noorah akabadilisha jina na kuitwa Camila.”
Tunampa pole Noorah kwa msiba huo.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
03 Mar 2015

Post a Comment

 
Top