Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mwenyekiti mpya wa Kamati ya PAC, Amina Mwidau (Viti Maalumu Mkoa wa Tanga CUF).


Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Tanga, Bi.Amina Mwidau (CUF) ndiye Mwenyekiti mpya wa Kamati ya PAC baada ya aliyekuwa mwenyekiti wake, Bw.Zitto Kabwe kung'atuka kwenye nafasi yake ya ubunge.
Kupitia akaunti yake ya Facebook, aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema) na Mwenyekiti wa Kamati ya PAC ambaye jana March 21,2015, alijiunga rasmi na Chama cha ACT-Tanzania, Zitto Kabwe amempongeza Amina kwa imani aliyopewa na wajumbe wenzake wa Pac.

"Nimefanya kazi na Amina tangu mwaka 2010 tulipokuwa kamati ya POAC na nina imani, kwa ushirikiano mkubwa wa Makamu Mwenyekiti ndugu Deo Filikunjombe wataendeleza kazi tuliyoianza ya kujenga mfumo madhubuti wa Uwajibikaji nchini kwetu" aliandika Zitto Kabwe.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
22 Mar 2015

Post a Comment

 
Top