Mamia ya wananchi wa Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, jana walijitokeza kuuaga mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mbinga-Magharibi, Kapteni John Komba ambao uliwasili majira ya saa 10.25 katika Uwanja wa Ndege wa Ruhuwiko, mjini hapa.
Baada ya mwili huo kuwasili kwa ndege ya kukodi mkoani hapa, ulipokelewa na viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa na serikali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mark Mwandosya pamoja na baadhi ya wabunge wa Mkoa wa Ruvuma huku baadhi yao wakiangua vilio kiwanjani hapo.
Baadaye mwili huo lipelekwa katika uwanja wa michezo wa Majimaji ambapo wananchi walipata fursa ya kuuaga na kisha kuelekea kijijini kwake Lituhi kwa ajili ya mazishi ambayo yamefanyika leo.
Msafara huo kutokea uwanja wa ndege uliongozwa na pikipiki magari ya watu binafsi sambamba na vikosi vya ulinzi na usalama huku wananchi wakiwa wamejipanga barabarani kushuhudia mwili huo.
Awali, kabla ya mwili wa Komba haujaingia uwanjani, waliupitisha katika mitaa mbalimbali ya Manispaa ya Songea kwa lengo la kutoa nafasi kwa wananchi ambao hawataweza kufika uwanjani, wapate fursa ya kuaga.
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu alisema hadi mwili unawasili, bado wananchi hawakuwa wakiamini kilichotokea kwa kumpoteza mtu muhimu, makini na mbunifu na mwenye vionjo vya muziki.
Alisema, Komba alikuwa mtu wa watu wote mwenye upendo na mpenda maendeleo na kwamba kifo chake kilikuwa ni cha kushtukiza.
Aliwataka wananchi mkoani Ruvuma kuwa watulivu na watakaobahatika kwenda kuzika kijijini, walitakiwa kuwahi kabla ya Rais Jakaya Kikwete hajawasili Lituhi.
Rais Kikwete, leo ameongoza mamia ya wananchi kwenye mazishi ya Kepteni Komba ambapo ilitangulia ibada ya Misa Takatifu iliyoongozwa na Askofu wa Jimbo la Mbinga, John Ndimbo.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- Tetemeko Lililotokea Jana Katika Mikoa Ya Kanda ya Ziwa Limeua Zaidi ya Watu 10 na Kujeruhi Wengine 12011 Sep 20160
Tetemeko la ukubwa wa mtikisiko wa kipimo cha Ritcher 5.7 limetokea katika mikoa mitatu nc...Read more ?
- Uteuzi mwingine wa Rais Magufuli leo September 9 201609 Sep 20160
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo September 09 201...Read more ?
- Viongozi wa Afrika Mashariki Waigomea Ulaya....Wajipa Miezi Mitatu Kuutafakari Mkataba wa EPA09 Sep 20160
JUMUIYA ya Afrika Mashariki (EAC), imeiomba Jumuiya ya Ulaya (EU), iipe muda wa miezi mitatu kuju...Read more ?
- Msafara wa Makamu wa Rais, Samia Suluhu wapata ajali Mtwara.09 Sep 20160
Msafara wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mama Samia Suluhu Hassan ambao uliku...Read more ?
- Majibu ya Waziri mkuu Majaliwa Leo Bungeni kuhusu wahusika wa mauaji ya askari08 Sep 20160
Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania inaendelea kukutana na wadau tofauti wanaohusika na ...Read more ?
- Makamu wa Rais: Viongozi Na Watumishi Wa Umma Kuchukuliwa Hatua Kali Iwapo Watabainika Kukiuka Taratibu Za Kazi08 Sep 20160
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameiagiza Sekretarieti ya M...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment