Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Msanii wa filamu Wastara Juma, ambaye ni mjane wa aliyekuwa staa wa filamu mahiri nchini, Marehemu Sajuki Juma Kilowoko, ameweka wazi kuwa baada ya kufariki kwa mumewe, hakuna manufaa yoyote ambayo yanaendelea kupatikana katika filamu.

Wastara ameongezea kusema kuwa hakuna mafanikio ambayo yanaendelea kupatikana ama yanatarajiwa kupatikana kwake na familia kutokana na mfumo wa biashara hiyo ya filamu.
 
Wastara amesema kuwa, kazi ambazo Marehemu ameziacha na nyingine nyingi za filamu huuzwa kwa wasambazaji na hakimiliki zake zote na hivyo kuendelea kusambazwa miaka na miaka bila msanii kufaidika na chochote kama ilivyo kwa kazi za Marehemu Sajuki.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top