June 19, 2025 06:23:52 PM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Stori: Musa Mateja/Risasi
ICON wa Bongo Fleva Nasibu Abdul ‘Diamond’,  juzikati aliamua kumtolea uvivu, aliyewahi kuwa mpenzi wa mwandani wake wa sasa, Zarinah Hassani ‘Zari’, King lawrenc kwa kumuita mpuuzi anayetafuta kiki kwa vile kila kukicha kazi yake ni kumfuatafuata kwa maneno ya kejeli na kumtusi.

X wa Zari, King lawrence akipozi.
Akipiga stori mbili tatu na gazeti hili hivi karibuni, staa huyo alisema mara nyingi amejitahidi kumpuuza kwa kitendo chake cha kumkejeli katika mitandao ya kijamii, lakini kitu alichogundua ni kwamba mpenzi huyo wa zamani wa Zari anataka yeye amjibu ili aweze kulikuza jina lake, kitu ambacho  ni cha kijinga.

Zarinah Hassani ‘Zari’.
“Nimejitahidi sana kukaa kimya kila anaponitusi huyu jamaa, lakini kumbuka mimi ni binadamu, najaribu kuliangalia jambo hili nagundua kwamba hana chochote cha msingi anachoongea zaidi ya matusi,  anatafuta nimjibu kitu ili apate kiki aweze kutimiza ndoto zake,” alisema Diamond na kuongeza:

ICON wa Bongo Fleva Nasibu Abdul ‘Diamond’ akiwa na Zari.
“Nashukuru nimegundua hana mada ya kuzungumza katika mitandao zaidi ya mimi na Zari, ningemshauri aendelee na shughuli zake za kila siku, asihangaike na kitu asichokijua, kugombana na mimi ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa, mimi nawaza nifanyeje ili niweze kuitangaza nchi yangu, yeye anawaza afanyeje ili aweze kupandisha jina lake, siwezi kubishana na mpuuzi.”
Mwanaume huyo Mganda, kwa muda mwingi amekuwa akiweka picha zake, Zari na Diamond akisindikiza na maneno ya kejeli na dhihaka dhidi ya mkali huyo wa Bongo Fleva, katika kile kinachoonekana kuwa ni kushikwa na wivu.
~GPL
Bonyeza hapa chini kuona zaidi

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
31 Jan 2015

Post a Comment

 
Top