Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mchoro wa mkia wa ndege ukionyesha kifaa cha kutunza kumbukumbu za ndege 'black box'.
Picha ikionyesha mabaki ya ndege ya AirAsia kutoka baharini.
Kikosi cha uokoaji kikikusanya baadhi ya mabaki ya ndege ya AirAsia.
MKIA wa Ndege ya AirAsia QZ8501 iliyopotea na watu 162 Desemba 28, mwaka jana umepatikana leo katika Bahari ya Java, Indonesia.
Eneo la mkia ndipo kifaa cha kutunza kumbukumbu za ndege 'black box' kinapatikana na upatakianaji wake utasaidia wachunguzi kubaini chanzo cha ndege hiyo kupotea na kisha kuanguka baharini.
Ndege hiyo ilikuwa ikitokea Jiji la Surabaya nchini Indonesia kuelekea Singaporea. Mpaka sasa miili 40 imeopolewa kutoka baharini katika eneo ambalo ndege hiyo ilianguka.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top