June 19, 2025 03:44:59 AM Menu
 

Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
WAKATI baadhi ya wasanii wakipewa masharti kuacha kuigiza pindi wanapoolewa, nyota wa Bongo Movies, Salma Jabu ‘Nisha’, amedai hata kama akiamua kuolewa na kuishi na mwanaume kamwe hawezi kuachana na tasnia hiyo kwani ndiyo iliyomfanya aishi maisha mazuri mjini.

 
Nyota wa Bongo Movies, Salma Jabu ‘Nisha’.

Nisha alizungumza na paparazi wetu juzikati na kudai kuwa wanawake wengi wamekuwa maskini kwa kuwa wanashindwa kuendelea na kazi walizokuwa wakizifanya awali kutokana na kubanwa na wanaume ambao hawana malengo ya maisha.

“Sidhani kama atatokea mwanaume atakayesema eti acha filamu ndiyo uwe mke wangu, wapo ambao walileta ujinga huo na wakaishia njiani kwa sababu hawana jambo geni, maisha yangu yamejengwa na filamu na ndiyo kazi inayonipa kila ninachokitaka, siiachi,” alisema Nisha.
Ungana nasi katika Facebook na Umechekeshwa

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro
13 Dec 2014

Post a Comment

 
Top