Takriban watu 36 wameuwa kwenye machimbo huko Koromei kwenye kaunti ya Mandera, leo asubuhi na wanamgambo wa kundi la Al-Shabaab.

Watu wote waliouwa sio waislamu. Baadhi ya watu waliopona wamewaambia polisi kuwa waislamu waliokuwa kwenye eneo hilo waliachiwa.
Wahanga hao waliambiwa kusimama kwenye mstari na wengi walipigwa risasi kichwani na wengine walichinjwa. Polisi wamesema watu hao walishambuliwa wakiwa wamelala mida ya saa saba usiku.
November 22, wanamgambo hao pia waliishambulia basi na kuwaua abiria 28 kwenye kaunti ya Mandera. Watu hao pia walipigwa risasi kichwani.
Chanzo: Daily Nation
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment