Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Lori aina ya Scania namba T 607 CWV Semi Taller (kama linavyoonekana katika picha) lililokuwa limebeba kokoto limeanguka katikati ya lami muda huu katika eneo la Chalinze Mzee Mkoani Pwani na kuharibika vibaya.



Kwa  mujibu wa Mashuhuda, ajali hiyo ametokea baada ya gari hilo lililokuwa likielekea Dar es Salaam, kuteleza kutokana na mvua iliyonyesha asubuhi ya leo mkoani humo.
 Hata hivyo askari wa usalama barabarani wamefika eneo la tukio na kufanikiwa kuliondoa gari hilo ambalo limesababisha foleni kubwa ya magari yaliyokuwa yakitokea jijini Dar es Salaam kwenda mikoa ya Tanga, Kilimanjaro na Arusha kutokana na kuziba barabara.




Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top