Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Madaktari wa mwanzo wa Cuba walipowasili Freetown

Rais wa zamani wa Cuba, Fidel Castro, anasema nchi yake itatuma karibu madaktari na wauguzi 300 zaidi kusaidia kupambana na Ebola Afrika.

Alisema Cuba iko tayari kushirikiana na Marekani kwa masilahi ya amani duniani.
Cuba imeshatuma madaktari na wauguzi 165 huko Afrika Magharibi.
Katika tukio jengine, Shirika la Afya Duniani, WHO, limesema kuwa ripoti yake ya siri iliyofichuliwa nje ya shirika, ambayo ilidai kuwa shirika hilo lilifanya makosa katika kushughulikia janga hilo la Ebola, haikuwa kamilifu na ilikuwa bado haikuchambuliwa.
WHO imesema uchambuzi kamili wa hatua ilizochukua utakamilika baada ya ugonjwa wa Ebola kudhibitiwa.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top