KWAKO Miss Sitti Mtemvu mwakilishi wa Wilaya ya Temeke na sasa wewe ni Redds Miss Tanzania 2014.
Vipi uko poa? Raha ya ushindi unaionaje? Najua sasa hivi bado hujatulia, unatafakari kwa makini juu ya shilingi milioni 18 ulizokabidhiwa kama mshindi, tafakari mama, ndiyo muda wake.
Ukitaka kujua hali yangu, mimi ni mzima wa afya, namshukuru Mungu.
Hongera kwa ushindi uliopata japo nimesikia kuna baadhi ya watu
hawakukubaliana na matokeo.
Huo ndiyo ushindani, lazima kila mmoja awe na mtazamo wake lakini mwisho wa siku, hawakatazwi kusema na inawezekana pia wana hoja.
Huo ndiyo ushindani, lazima kila mmoja awe na mtazamo wake lakini mwisho wa siku, hawakatazwi kusema na inawezekana pia wana hoja.
Moja kwa moja nikiachana na salamu, nataka kuzungumza na wewe
kuhusiana na maisha yako baada ya huo ushindi wa kishindo ulioupata
usiku wa Oktoba 10, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Mlimani City jijini
Dar.
Yawezekana uliwaza kabla au hukutarajia kushinda lakini tayari
umeshatangazwa wewe ndiye mshindi. Swali langu la msingi kwako ni je,
umejipangaje baada ya ushindi huo?Hautabaki historia ya mara moja na
kusahaulika kama wenzako? Kumbukumbu inaonyesha wapo wenzako wengi
waliopotea ndani ya muda mfupi tu baada ya ushindi.
Hatukuwasikia tena wakifanya mambo mbalimbali ya kijamii au kuanzisha
taasisi mbalimbali ambazo zitamfanya azidi kuonekana muhimu katika
jamii. Kutwaa ubingwa na kukaa kimya, kunapoteza maana kabisa ya
ushindi.
Sijachelewa, taji ndiyo kwanza la motomoto. Weka mikakati yakinifu,
jiwekee malengo ya taji lako na fedha ambazo umekabidhiwa. Wekeza katika
miradi mbalimbali, wewe mwenyewe ni wakati wako wa kutumia fursa au
vipaji mbalimbali ambavyo vinaweza kubebwa na taji lako, ukavionyesha na
Watanzania wakakuunga mkono.
Nikirudi kwako Mkurugenzi wa Lino International Agency, Hashim
Lundenga, hizi kasoro za sijui matokeo yamepangwa, mshindi alijijua
kabla, mshindi kukosea maelekezo ya majibu na mambo mengine kwa nini
viendelee kuwepo?
Achana na yale mabango ya Sitti ambayo yalionekana yakionyesha kwamba
ni mshindi pale ukumbini kabla ya kutangazwa, lakini vipi kuhusu lile
gari la Hammer ambalo lilikuja maalum kwa ajili ya kumpokea mshindi,
walijua kama atashinda nini? Lundenga wewe!!
Nafikiri ni wakati sasa wa kubadili gia katika sura nzima ya
mashindano hayo kwani ninavyoona mimi, msisimko wake unaendelea kupungua
siku hadi siku. Tunahitaji shindano hili liboreshwe ili tuwe tunampata
mshindi atakayekwenda kuchuana na kushinda Miss World na siyo kila siku
ziwe blablaa tu!
Wasalaam, Erick Evarist.
Bonyeza Hapa
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment