NINAMFAHAMU
Blandina Changula maarufu kama Johari, tokea akiwa underground wa
maigizo katika kikundi cha Kaole, kabla hajapata jina linalomfanya kuwa
mmoja wa wakongwe katika filamu Tanzania.
Johari anaweza kutoa machozi wakati wowote akitaka. Anaweza kucheka
kwa sauti na furaha dakika hii, lakini inayofuata akatoa machozi mengi
hadi unashangaa. Napata wasiwasi ninapomuona akitoa machozi katika
misiba, hujiuliza kama analia kweli kwa uchungu au ni mbwembwe tu za
maigizo ili watu wajue ana uchungu!
Kama nilivyosema mwanzo, Johari ni mmoja kati ya waigizaji wasichana
ninaowafahamu zaidi katika fani, pengine kuliko masistaduu wengi
waliopata majina makubwa katika miaka ya hivi karibuni. Anajua kufanya
kazi kwa kweli na ni lazima hawa waliomkuta, wampe heshima anayostahili
kwa sababu anao mchango mkubwa sana katika game.
Ninafahamu kwamba Vicent Kigosi, wakati huo naye akianza kuogelea
kwenye umaarufu wa filamu, alikuwa akitoka na dada huyu. Mara kadhaa
nimewahi kuwakuta pamoja na kwa maana hiyo, hakuna mdau asiyetambua
uhusiano wao.
Ni kutokana na uhusiano huo, ambao awali ulionekana kama wenye
mwelekeo wa kuzaa ndoa, wawili hao walifungua kampuni yao, RJ, kila
herufi ikiwakilisha mwanzo wa majina yao ya kisanii.
Lakini kama tunavyofahamu, wawili hawa walianza chokochoko katika uhusiano wao, baada ya kuwepo kwa taarifa za Ray kuchepuka na Chuchu Hans, binti mdogo aliyemkuta Johari katika fani. Mwanzo ilikuwa ni siri, lakini baadaye ikathibitika kuwa ni kweli kiasi kwamba hata Johari akakubali na kumwaga manyanga.
Lakini kama tunavyofahamu, wawili hawa walianza chokochoko katika uhusiano wao, baada ya kuwepo kwa taarifa za Ray kuchepuka na Chuchu Hans, binti mdogo aliyemkuta Johari katika fani. Mwanzo ilikuwa ni siri, lakini baadaye ikathibitika kuwa ni kweli kiasi kwamba hata Johari akakubali na kumwaga manyanga.
Sijui, labda kwa sababu ni wasichana, wawili hawa wamekuwa wakipigana
vijembe kila wanapokaa pamoja au kukutana. Mara moja waliwahi
kuripotiwa kupigana katika ofisi za RJ.
Wiki iliyopita, wawili hawa waliripotiwa kutukanana kwa mara nyingine na almanusura wazichape. Walikutana katika eneo ambalo Johari alikuwa ameweka kambi yake, Chuchu akiwa ameambatana na Ray.
Wiki iliyopita, wawili hawa waliripotiwa kutukanana kwa mara nyingine na almanusura wazichape. Walikutana katika eneo ambalo Johari alikuwa ameweka kambi yake, Chuchu akiwa ameambatana na Ray.
Niseme wazi kuwa ingawa ni vigumu kuzungumzia hisia za watu
kimapenzi, lakini kwa uzoefu wa wawili hawa, inaonekana kama wanaishi
maisha flani yanayokwenda kinyume na ustaarabu wa kisasa.
Nianze na Chuchu. Mara zote ugomvi unapotokea, binti huyu huwa amemfuata Ray katika eneo analojua kabisa kuwa Johari atakuwepo, hivi kwa kutumia tu busara zake za kawaida, kwa nini huwa hajiepushi kusogelea? Kwa sababu anajua kuwa yeye alimpora mwenzake mtu wake.
Nianze na Chuchu. Mara zote ugomvi unapotokea, binti huyu huwa amemfuata Ray katika eneo analojua kabisa kuwa Johari atakuwepo, hivi kwa kutumia tu busara zake za kawaida, kwa nini huwa hajiepushi kusogelea? Kwa sababu anajua kuwa yeye alimpora mwenzake mtu wake.
Hivi anapokwenda ofisini kwa Ray kwa mfano, akijua kabisa Johari pia
yupo, haoni kama anayakaribisha matatizo makusudi? Maana yake ni kuwa
anakwenda pale akitamba kwamba hawezi kufanywa lolote!
Na Johari, kwa umri ulionao, huoni kama ni kujifedhehesha tu
kumpigania mwanaume unayejua kabisa hana mapenzi nawe? Huhisi watu
wanaweza kukuona ni mshamba wa mapenzi?
Binafsi, ninaamini kama ungekuwa huna habari nao, wao ndiyo wangejisikia vibaya na pengine wangekuwa wanajisikia aibu kuibuka sehemu ulipo kwa vile watasanifika.
Binafsi, ninaamini kama ungekuwa huna habari nao, wao ndiyo wangejisikia vibaya na pengine wangekuwa wanajisikia aibu kuibuka sehemu ulipo kwa vile watasanifika.
Sasa wanapofikia sehemu wanapigana na kutukanana hadharani, sidhani
kama kuna mshindi kati yao zaidi ya wastaarabu kuwaona kama watu
wanaotafuta kiki, kama wenyewe wasanii wanavyosema.
Kwa majina na umaarufu walionao, walipaswa kuwa mfano. Kila siku watu wanadai wanawake ni dhaifu, lakini kwenye majukwaa wanakanusha sana ili hali katika uhalisia wanathibitisha. Kwetu sisi wanaume, tukishaamua kuachana na mwanamke, hatunaga bifu tena na mwanaume mwingine atakayekwenda kujitwisha mzigo!
Kwa majina na umaarufu walionao, walipaswa kuwa mfano. Kila siku watu wanadai wanawake ni dhaifu, lakini kwenye majukwaa wanakanusha sana ili hali katika uhalisia wanathibitisha. Kwetu sisi wanaume, tukishaamua kuachana na mwanamke, hatunaga bifu tena na mwanaume mwingine atakayekwenda kujitwisha mzigo!
Ushauri wangu kwa hawa wadogo zangu ni kujitambua, Johari kwamba enzi
zake kwa Ray zilishamalizika na Chuchu kwamba kwa kuwa huyu ni wako,
acha kumfuata mwenzio katika anga zake!
BONYEZA HAPA
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment