Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
iMiezi miwili baada ya kumalizika kwa michuano ya kombe la dunia, huku timu ya taifa ya Ujerumani ikitwaa ubingwa wa dunia, nahodha wa timu hiyo Philip Lahm alifikia uamuzi wa kujiuzulu kuichezea timu hiyo na hivyo kuacha wazi nafasi ya unahodha kwenye timu hiyo,
Leo hii wiki kadhaa baada ya Lahm kujiuzulu, kocha wa timu ya taifa ya Ujerumani Joachim Low amemteua nahodha mpya wa timu hiyo.
Kiungo wa FC Bayern Munich  Bastian Schweinsteiger ndio amerithi nafasi iliyoachwa wazi na Philip Lahm.
Bastian mwenye miaka 30 ameshaichezea Ujerumani kwenye mechi zaidi ya 100 tangu alipoanza rasmi kuitumikia timu hiyo mwaka 2004.
Manuel Neur pia ameteuliwa kuwa nahodha msaidizi wa Ujerumani.
  • Bonyeza Hapa

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top