Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This





Pistorius amekanusha kumuua mpenzi wake kwa maksudi
Kundi la mawakili wanaomtetea mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini Oscar Pistorius wanasema kuwa viongozi wa mashitaka wamevuruga kesi hiyo kwa minajili ya kumfanya kuwa na makosa
Kwenye taarifa yake ya mwisho wakili wa Pistorius Barry Roux amesema kuwa bwana Pistorius angefunguliwa mashitaka ya kuua bila kukusudia bali si ya mauaji baada ya kumpiga risasi na kumuua mpenziwe Reeva Steenkamp.
Bwana Pistorius anasema kuwa alimpiga risi kimakosa akidhani kuwa alikuwa ni jambazi.
Lakini bwana Roux alikiri kwamba Pistorius anapaswa kupatwa na hatia kwa kosa la kutumia silaha yake katika mgahawa.

Wakati kila upande utakapokamilisha kutoa kauli zao ya mwisho jaji ataahirisha kesi hiyo kwa takriban wiki moja kufanya uamuzi.
Mwanariadha huyo amekanusha makosa yake dhidi yake ikiwemo kosa la kutumia silaha yake katika sehemu ya umma pamoja na kumiliki silaha haramu.
>>>>BBC
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331 
 
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa 

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top