MBONGO-Fleva anayefanya poa na ngoma yake ya Nitasubiri, Juma Mussa ‘Jux’ na staa mwenzake ambaye ana kofia nyingine ya utangazaji, Vanessa Mdee ‘V-Money’ wanadaiwa kuwa ni wapenzi.
Juma Mussa ‘Jux’ akiwa na Vanessa Mdee ‘V-Money’ wanaodaiwa kuwa ni awapenzi.
Madai ya wawili hao kuhusishwa kimapenzi yameendelea kujidhihirisha siku hadi siku na zaidi ni hivi karibuni walipokutana kwenye ziara ya Serengeti Fiesta 2014 mkoani Kagera na Tanga, ambapo muda mwingi walionekana kugandana kama luba hadi wenzao kudai kuwa walikuwa hata wakilala chumba kimoja hotelini.
Katika kuwafuatilia, paparazi wetu alifanikiwa kupata baadhi ya picha za matukio yao yaliyoonesha michakato na harakati zao za kimalovee zinavyokuwa siku zote.
Wakiteta jambo.
Jux na Vanessa, wakiwa mkoani humo walionekana muda mwingi wakiwa pamoja kwenye gari walipokuwa wakienda kumuona Babu Njenje na wakati wakiwa wanaelekea Uwanja wa Mkwakwani kwenye shoo.
Hata baada ya Jux kushuka stejini, alionekana akiwa amekaa ‘very close’ na Vanessa huku wakiwa kwenye mazungumzo yaliyodaiwa ni ya kimahaba niue.
Wakiwa pamoja kama kumbikumbi.
Mpaparazi alifanya jitihada za kuzungumza na Jux juu ya uhusiano wao, lakini jamaa huyo alimchomolea kwa kusema kwamba hayuko tayari kuzungumzia ishu hiyo kwani Vanessa ni mshikaji wake tu na hakuna kibaya juu yao zaidi wanafanya kazi pamoja tu.
“Kiukweli sihitaji kuzungumza lolote juu yangu na Vanessa ila ni mwanamuziki mwenzangu hivyo tunafanya kazi pamoja,” alisema Jux.Vanessa kwa upande wake alipoulizwa juu ya ishu hiyo, alimtaka mpaparazi ‘kuipotezea’ habari hiyo kwani si muhimu kwa sasa.
Mbali na Vanessa, Jux aliwahi kudaiwa kutoka na mwigizaji Jacqueline Wolper na modo Jacqueline Patrick huku Vanessa naye akiwa alisharipotiwa kutoka na Omary Nyembo ‘Ommy Dimpoz’.
jux na modo Jacqueline Patrick
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Je Umezisoma Hizi?
- VIDEO: Mama Wema Aeleza Beef yake na Man Fongo Kisa……..09 Sep 20160
NI Mama Wema Sepetu ambae ameingia kwenye headlines mitandaoni baada ya kutofautiana na mkali wa ...Read more ?
- Busu la Nelly Kamwelu shavuni kwa Diamond akiwa na Wizkid lawatoa povu mashabiki (Video)25 Aug 20160
Haipiti wiki bila Diamond kuwatoa povu mashabiki, hata kama alichokifanya si kwamba alidhamiria...Read more ?
- Picha za Masanja na Mke wake Zazua Maswali Kwa Mashabiki wake..Wadai Mke wa Mchungaji Apaswi Kuvaa Hivyo19 Aug 20160
Baada ya Harusi ya Mchekeshaji Masanja na Mkewe iliyofungwa Jumapili iliyopita wawili hao wameon...Read more ?
- AUDIO: Kitu Diamond kasema kuhusu yeye kuwa mapenzini na Hamisa Mobetto03 Aug 20160
Ukaribu wako kwenye mitandao ya kijamii siku za karibuni unaweza kuwa ulikukutanisha na stori...Read more ?
- Shamsa Ford Amuweka Wazi Mpenzi wake Mpya03 Aug 20160
Msanii wa filamu nchini Shamsa Ford amefunguka na kusema kuwa baada ya kuachana na mpenzi wake wa...Read more ?
- Madai: Flora Amwangukia Mbasha30 Jul 20160
Habari ya mjini ni Mwimba Injili Bongo, Flora Mbasha kudaiwa kumwangukia mumewe waliyetengana, Em...Read more ?
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Post a Comment