Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Jeshi la Polisi linamshikilia  Raia wa  Vietnam Dong Van(47) kwa kumkamata akiwa na meno 65 na kucha 447 za Simba kinyume cha sheria vyenye thamani ya Shilingi Milioni 189,420,000.


Kamishna Msaidizi  wa Polisi wa Uwanja wa  Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,  Hamisi Selemani, amesema mtuhumiwa huyo alikamatwa jana wakati alipotaka kusafirisha nyara hizo kwa kutumia Shirika la Ndege la Qatar Airways kwenda nchini Vietnam kupitia Doha.

Amesema alipopekuliwa alikutwa na nyara hizo ambazo alizihifadhi kwenye 

pakiti 7 za kahawa na pakiti moja ya mchele  na kuzichanganya na pakiti nyingine 15 za vyakula vya aina mbalimbali

Kamanda Selemani amesema  pakiti hizo ziliwekwa ndani ya begi la nguo ili kupoteza ushahidi wa aina ya mzigo alioubeba kwa wakaguzi wa uwanjani hapo.

Aidha amesema mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani mara baada ya uchunguzi kukamilika ili aweze kuchukuliwa hatua za kisheria.
Chanzo Times Fm.co.tz
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331

kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa
 

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top