Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


Dar es Salaam. Raia wa China, Pianan Li (51), amekamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), akiwa na mifupa miwili ya twiga na fuvu la kichwa cha swala likiwa na pembe zake.
Li alikamatwa juzi saa 10 jioni alipokuwa akijianda kwa safari kuelekea China kwa kutumia ndege ya Shirika la Qatar kupitia Doha ambapo alikutwa na nyara hizo alizoficha kwenye begi la nguo. Kamanda wa Polisi Viwanja vya Ndege, Hamisi Selemani alisema raia huyo wa China alikuwa hana kibali chochote kinachoonyesha uhalali wa kuzisafirisha nyara hizo nje ya nchi.
“Alidai kuwa nyara hizo alitokanazo Afrika Kusini, lakini polisi wa uwanja walipodai vibali hakuwa navyo,” alisema na kuongeza:
“Baada ya kupita kwenye mashine ya ukaguzi tulibaini ameweka nyara hizo kwenye begi la nguo na tulikuta amezifunga vizuri kwenye nguo zake.”
Alisema kwa hali ya kawaida, mtu anapokuwa na nyara hizo lazima apewe kibali kutoka nchi husika, lakini walimshangaa raia huyo akidai kuwa ametoka nazo Afrika Kusini.
Selemani alisema mtuhumiwa huyo aliyekuwa na hati ya kusafiria ya China, alihojiwa kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii na upelelezi unaendelea.
Selemani alisema polisi wataimarisha ulinzi katika maeneo ya mipakani na viwanja vya ndege ili kudhibiti aina hiyo ya utoroshaji wa nyara.
Hivi karibuni Raia wa Vietnam, Dong Van (47) alikamatwa katika uwanja huo akiwa na meno 65 na kucha 447 za simba zenye thamani ya Sh189.4 milioni.
Alikamatwa na nyara hizo akiwa amezificha kwenye begi lake la nguo, huku zikiwa zimefungwa vizuri katika pakiti za mchele na kahawa.
>>>>>Mwananchi
  • Bonyeza Hapa

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top