Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Baada ya gari la muigizaji maarufu wa filamu Bongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’ kukamatwa na polisi jijini Dar es Salaam likihusishwa na tukio la ujambazi linalodaiwa kutokea Kijitonyama, amezungumzia nini kinaendelea kwenye madai hayo. 

Akizungumza na Bongo5 leo, Dude amesema kuwa ni kweli gari yake imedaiwa kuhusishwa na tukio hilo lakini uchunguzi unaendelea wa kuwatafuta wahusika aliyokuwa amewaachia gari hilo.   

“Siwezi kulizungumzia suala hili kwa sababu uchunguzi unaendelea na polisi, lakini gari yangu inadaiwa kukamatwa kwenye tukio la ujambazi,” amesema. 
“Kuna madogo walikuwa nayo hiyo gari, kwasababu nilikuwa naiuza kwahiyo hao madogo ndio walikuwa nayo. Lakini siwezi kulizungumzia suala hili kwa sababu kuna mtu wanamtafuta mpaka wamkamate ndo tujue hii kweli ilikuwaje. Kwahiyo kulielezea hili naonekana kama naharibu upelelezi wa polisi. 



Mimi hawakunikamata nilienda kwa sababu waliniita nikaenda kutoa tu maelekezo nikaachiwa. Sema tu gari yangu imeharibiwa kwa sababu wale vijana walipiga kelele za wizi wananchi wakabonda bonda lile gari. Nadhani kuanzia Jumatatu au Jumanne ninaweza nikalielezea hili kwa mapana zaidi kwa sababu nitakuwa nimeshajua polisi wanaendeleaje.”


Kwa mujibu wa Global Publisher, gari hilo lilihusishwa na tukio la ujambazi linalodaiwa kutokea Kijitonyama Mpakani usiku wa saa 5.15 Julai 21 mwaka huu ni aina ya Vitz lenye namba za usajili T 360 BAJ. 
 
 Lilikutwa likiwa na vijana wawili ndani yake, waliotajwa kwa majina ya Seif Jafari na Longina Ramadhani, waliotaka kupora Bajaj yenye namba za usajili T 296 CSC iliyokuwa ikiendeshwa na Seleman Khalfani.

UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331
 
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa


Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top