Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


Nairobi-Kenya-International-Airport
Mwanamume mmoja Raia wa Nigeria imebidi alazwe kwenye hospitali ya taifa ya Kenyatta Nairobi Kenya baada ya kugundulika alikua na mzigo wa dawa za kulevya wa vidonge 57 tumboni mwake.Huyu jamaa alikua anazisafirisha hizi dawa kutoka Lagos kwenda Bangkok lakini ghafla akaanza kupata maumivu baada ya kuchelewa kufikisha mzigo aloubeba tumboni mwake baada ya ndege waliyokua wakisafiria kutua Nairobi kwa dharura.
Ilitua kwa dharura baada ya rubani kuumwa ghafla hivyo kulazimu ndege kutua Nairobi kisha abiria wote kupelekwa hotelini na hapo ndio Mnigeria huyu akaanza kuhisi maumivu makali tumboni.


Aeroplane landing at sunset, Canada
Simon Ithae ambae ni mkuu wa mawasiliano hospitali ya Kenyatta amesema ‘alitueleza amemeza vidonge na alikua akiamini ndicho chanzo cha maumivu hivyo alipoona hawezi kustahamili aliita Polisi akidai ameumizwa na anahitaji kupelekwa hospitali lakini lengo lake ni apange njama na madaktari kutoa dawa za kulevya bila yeye kukamatwa na aendelee nazo na safari lakini mipango yake haikufanikiwa kwa sababu Madaktari walimpa chakula ili kutoa dawa hizo na kisha wakawapa taarifa Polisi.
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top