Huku
harakati za kutaka matumizi ya Bangi kuhalalishwa zikishika kasi katika
sehemu mbali mbali duniani, Tanzania haijaachwa nyuma.
Wanakijiji
katika wilaya ya Makete , mkoa wa Njombe Kusini Magharibi mwa Tanzania
wanataka serikali iweke sheria ambayo itaweza kuhalalisha matumizi ya
mmea huo.
Mwenyeketi
wa Halmashauri ya wilaya ya Makete Daniel Okoka amesema matumizi ya
Bangi katika wilaya hiyo hayajaanza leo, tangu zamani watu kitamaduni
walikuwa wakitumia Mbegu za Bangi kukaanga na chakula.Wanakijiji hao
zamani walikuwa wakitumia mbegu za mmea huo kukaanga na chakula lakini
siku hizi wanalazimika kuzitumia kwa usiri mkubwa wakihofia kukamatwa na
polisi.
Na kama mmea huo ungekuwa na tahri kubwa kiafya, basi watu wengi wilayani humo wangekuwa vichaa.
Miti ya mimea hiyo pia ilikuwa ikitumiwa kutengeza kamba ambazo anasema zilikuwa za nguvu sana.
Lakini kwa sababu ya sheria kali, matumizi ya Bangi au Marijuana yanafanywa kichinichini katika wilaya hiyo.
>>>>>BBC
UKIONA TUKIO LOLOTE LINATOKEA USISITE KUTUTUMIA PICHA KUPITIA WHATSAPP 0712-483 331
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu bonyza hapa
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Post a Comment
Post a Comment