|
Mwili umejaa
majeraha na makovu…… Mama wa kambo wa mtoto huyo Fidea Emmanuel aliiambia
Mwananchi kuwa mume wake alikuwa akimpa adhabu mtoto huyo mara kwa mara hasa
alipojisaidia au kukojoa ndani kwa kutumia fimbo ya mti wa m’buni.
Hata hivyo
mama huyo wa kambo na Erick alisema kutokana na hali mbaya ya mtoto huyo
iliyotokana na adhabu ya viboko,amekuwa akimtibu kwa kutumia dawa za mitishamba
bila ya kufanyiwa vipimo au kupelekwa hospitalini.
Pia, mtoto
huyo anaonekana kuwa na michirizi mikubwa katika sehemu ya kifua na tumbo
pamoja na makovu makubwa mwilini mwake, alama ambazo zinahusishwa na viboko
alivyokuwa akicharazwa na baba yake mzazi.
Naye,
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Maiga Audax Bayon, alisema kuwa ilikuwa ni vigumu
kumuona mtoto huyo kwa kuwa kila aliyemuulizia aliambiwa yuko ndani akijifunza
kusoma na watoto wengine jambo ambalo halikuwa kweli.
|
Post a Comment
Post a Comment