Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Mshambuliaji wa Timu ya Taifa ya Uruguay ,Luis Suarez ameibua mgogoro mkubwa huko Brazil baada kuonekana akimuuma Meno Beki wa Italia Giorgio Chiellini kwenye Mechi ya mwisho ya Kundi D la Fainali za Kombe la Dunia ambayo Uruguay waliitoa Italia kwa bao 1-0 (June 24, 2014) na wao kutinga Raundi ya Pili ya 16 bora.

 Tukio hilo lilitokea Dakika chache kabla ya Bao la Kichwa la Dakika ya 81 la Diego Godin kuwapa ushindi Uruguay.

Mara baada ya tukio hilo la kung’atwa, Chiellini aliinua Jezi yake kumwonyesha Refa  Marco Rodriguez wa Mexico ambae hakuchukua hatua yeyote.

Aprili 2013, Luis Suarez alifungiwa Mechi 10 kwa kumuuma Meno Beki wa Chelsea Branislav Ivanovic kwenye Mechi ya Ligi Kuu Uingereza.

Mwaka 2010 huko Uholanzi, Suarez alifungiwa Mechi 7 kwa kumuuma Kiungo wa PSV Eindhoven Otman Bakkal.
Giorgio akimuonyesha sehemu alipong'atwa meno na mshambuliaji wa Uruguay Luis Suarez refa kitendo hicho akukiona
Miaka minne iliyopita huko Afrika Kusini kwenye Fainali za Kombe la Dunia Suarez alizuia Mpira uliokuwa ukitinga Golini kwenye Dakika ya 120 kwa Mkono wake na yeye kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu, Ghana kupewa Penati ambayo Asamoah Gyan aliikosa na hatimae Uruguay kutinga Nusu Fainali kwa Mikwaju ya Penati.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top