UKATILI: MTOTO MLEMAVU AFUNGIWA NDANI NA MAMA YAKE KWA MIAKA 9 KOROGWE TANGA
Mtoto
mwenye ulemavu wa akili wilayani Korogwe, mwenye umri wa miaka 15,
amefungiwa chumbani na mama yake wa kambo kwa muda wa miaka 9, ambapo
amekuwa akijisaidia humo choo kikubwa na kidogo, kisha kuwekewa chakula
katika bakuli lake maalum ndani ya chumba hichoMwandishi
wetu ameshuhudia mtoto huyo akiwa chumbani na upande mmoja wa kanga
huku kukiwa na vinyesi na bakuli lake analowekewa chakula mithili ya
mnyama
.
Mama
mlezi wa mtoto huyo mlemavu aliyejulikana kwa jina la Khadija Makame
alipoulizwa kuhusu kitendo cha kumfungia ndani mtoto huyo, amesema kuwa
huwa anamtoa nje kwa chakula na hata kumsindikiza chooni, majibu ambayo
majirani walipingana naye baada ya kushuhudia ndani ya chumba chake
kukiwa na vinyesi na bakuli lake la kulia.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro








Post a Comment
Post a Comment