Blandina Chagula ‘Johari’, juzikati alifunguka
kwamba watu waachane na kusikiliza habari za
matapeli wa mapenzi, maana suala la Vicent
Kigosi ‘Ray’, kumvisha pete mchumba wake wa
sasa Chuchu Hans si la kweli na kwamba huo
ni utapeli
Akizungumza Ijumaa Mei 13, mwaka huu
Johari alisema hana taarifa zozote za Ray
kumvisha pete Chuchu na wala hatarajii
kusikia tukio la wawili hao kuoana
limefanyika.
“Mmh…unasema Ray kamvisha pete Chuchu...!
Hakuna jambo kama hilo wewe, achana na
matapeli maana hakuna ishu kama hiyo na Ray
hawezi kuoa kwa muda huu.”
“Kwani suala la kumvisha pete na kutoa
mahari lilifanyikia wapi maana kama kweli
kuna mazingira hayo basi atakuwa kafanya
kwa kificho sana.”
Na Musa Mateja,
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment