
Baadhi ya viongozi wanaowania urais nchini Malawi
Rais Joyce Banda wa Malawi
ameamuru kusitishwa mara moja kwa shughuli ya kuhesabu kura na kutangaza
matokeo ya uchaguzi mkuu wa nchi hiyo ulifanyika jumanne iliyopita.
Mwandishi wa BBC Baruan Muhuza amearifu kutoka mjini Lilongwe kuwa Dr Banda amesema amelazimika kuchukua hatua hiyo kutokana na kile alichokiita kuvurugwa kwa mtiririko mzima wa shughuli za upigaji kura,kuhesabu na hata namna ya kusimamia utoaji wa matokeo yake.
Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi ya Malawi Jaji Mackson Mbendera amesema kuwa anawasiliana na mwanasheria mkuu wa serikali ili kuangalia uwezekano wa amri hiyo ya Rais kutekelezwa na kama haijavunja sheria ya nchi.
>>>>>>>Chanzo bbcswahili
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment