| Gari ya polisi ikiingia katika hospitali ya wilaya ya Kahama kupeleka mwili huo |
| Baadhi ya wananchi wakishanga ajali hiyo awali mara baada ya kutokea |
Na Marco Mipawa, Kahama
Mtoto
wa kike anayekadiriwa kuwa na Umri wa miaka 7-10 jina na makazi yake
hayajafahamika, amefariki dunia baada ya kugongwa na gari wakati akivuka
barabara Kuu iendayo Rwanda katika eneo la Nyihogo wilayani Kahama
Mkoani Shinyanga.
Tukio
hilo limetokea jana majira ya Saa Nane na nusu mchana likihusisha gari
aina ya fuso Mitsubish lenye no T559 Mali ya Kuzenza John,lililokuwa
linaendeshwa na dereva Samwel Martine (38).
Kwa
mujibu wa mashuhuda, chanzo cha ajali hiyo ni mrundikano wa magari
yanayoegeshwa katika eneo la kisima cha mafuta cha Nyihogo sehemu
iliyowahi kusababisha zaidi ya ajali 5 hadi sasa.
Kufuatia
ajali hiyo wananchi walifunga barabara wakishinikiza serikali kuweka
matuta pamoja na kuondoa maegesho ya magari yaliyopo katika eneo hilo,
ili kuwapa nafasi waenda kwa miguu kuvuka barabara kwa usalama.
| Baadhi ya vipande vya magogo vilivyotumika na wananchi hao kufunga barabara hiyo kuu ya kwenda nchini Rwanda na Burundi |
Mkuu
wa kitengo cha usalama barabarani wilayani Kahama Robart Sewando,
amesema kwa sasa jeshi la polisi litaimarisha ulinzi katika eneo hilo,
ikiwemo kuzuia uegeshaji wa magari wakati taratibu zingine za Serikali
zikiendelea.
Jeshi
la polisi wilayani Kahama linamshikilia dereva wa gari hilo Samwel
Martine kwa mahojiano,ambapo mwili wa marehemu umehifadhiwa katika
chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya wilaya ya Kahama.
<<<<<BOFYA HAPA ULIKE PAGE YETU>>>>>
<<<<<BOFYA HAPA ULIKE PAGE YETU>>>>>
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment