Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Milionea: Messi amekubali kusaini mkataba mpya Barcelona ambao utamfanya awe mwanasoka anayelipwa zaidi ya wote duniani. 
 
MSHAMBULIAJI Lionel Messi atakuwa akilipwa Paundi Milioni 16.3 kwa mwaka katika mkataba mpya aliokubali kusaini na klabu yake, Barcelona jambo linalomfanya Muargentina huyo kuwa mwanasoka anayelipwa zaidi duniani. 

Baba wa mchezaji huyo Jorge alikutana na viongozi wa klabu hiyo Javier Faus na Antoni Rossich wiki iliyopita na kufikia makubaliano ya mkataba wa saba ndani ya miaka 11 ya mshindi huyo wa Ballon d’Or nne Barcelona. 
 
Messi atafikisha miaka 27 June na mkataba mpya unatarajiwa kuweka Camp Nou hadi mwaka 2018.
 
Kwa mshahara huo mpya, Messi anampiku hasimu wake, Cristiano Ronaldo wa Real Madrid ambaye analipwa Paundi Milioni 15 kwa mwaka.
<<<<<BOFYA HAPA ULIKE PAGE YETU>>>>>  

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top