Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
KIJANA Lalmohan Soren (17) amekata sehemu ya ulimi wake kwa wembe kutokana na imani kali ya dini kwa Mungu wake wa Kihindu. Soren aligundulika kukata sehemu ya ulimi wake nyakati za asubuhi alipokaa ndani ya msikiti wa Mahedevgarha katika eneo la Dugda, Jharkhand ndipo waumini walipoona damu imetapakaa sakafuni.

Waumini hao waliacha kusali na kuangalia zaidi ndipo wakakuta ulimi huo upo ndani ya bakuli pembeni ya Soren aliyekuwa hawezi kuzungumza. Sambamba na bakuli hilo waliona karatasi iliyoandikwa "nimeukata ulimi wangu na kuutoa kama sadaka kwa Mungu Shiva".

"Tafadhali msiniondoe hapa msikitini, nataka nikae hapa miguuni kwa Mungu".

Soren alitoa sadaka ulimi wake kwa Mungu Shiva kwa lengo la kumfurahisha na pia kutimiza ndoto zake. Kutokana na tukio hilo, kiongozi wa msikiti huo alitaarifiwa na akafanikiwa kumshawishi Soren akubali kupelekwa hospitali.

Madaktari walijaribu kuushona ulimi huo kwa lengo la kuurejesha sehemu ulipokuwepo awali, lakini walishindwa na baada ya siku chache Soren aliruhusiwa kutoka hospitalini.

Kwa sasa Soren yupo nyumbani na anaendelea kupona, lakini hawezi tena kuzungumza na amekuwa akipewa chakula cha majimaji. Hata hivyo, Soren mwenyewe hajutii kitendo alichokifanya na amekuwa akijivunia kwa ujasiri na kumfurahisha Mungu Shiva.
 
Kutokana na kitendo hicho, familia yake imeshtushwa, lakini imekubaliana na hali hiyo. Mama wa Soren anasema "mwanagu amekuwa akijihusisha na mambo ya dini tangu akiwa mtoto".

"Amekuwa akipenda dini sana, lakini sikuamini kama ipo siku atakata ulimi wake kumfurahisha mungu. Sijui kitakachotokea kwake lakini najua hataweza tena kuzungumza vizuri. Maisha yake ya baadaye yatamtegemea Mungu zaidi". Hata hivyo, mama huyo mwenye watoto wanne, ana uhakika Soren atapata baraka.

"Mwanangu amejitolea ulimi wake kumfurahisha mungu hivyo tuna hakika mungu atatimiza maombi yake yote na kumpa maisha mazuri", anasema mama huyo. Watu wa eneo hilo wameshangazwa na jinsi vyombo vya habari vilivyolichukulia suala hilo kwani wao wanaona ni kitu cha kawaida kutokea. Jirani wa Soren, Manoj Sharma anasema;

"watu wa eneo hili ni washirikina sana na siku zote wanatekeleza mambo ya ajabu. Mwaka 2011 kijana mmoja alijikata vidole viwili na kutoa sadaka kwa Mungu katika msikiti huohuo, hivyo tukio hili si jipya ingawa linaumiza nafsi za wengi."

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top