Timu ya Arsenal ya England imetwaa kombe la FA baada
ya kubamiza Hull City kwa jumla ya magoli 3 – 2 kwenye fainali
iliyofanyika katika uwanja wa Wembley siku ya jumamosi.
Katika mechi hiyo ya fainali Hull City ndio waliokuwa wa kwanza kuutikisa wavu wa Arsenal kwa magoli mawili ya haraka haraka yaliyofungwa ndani ya dakika 10 kipindi kwanza.

Katika kipindi cha pili Arsenal walikuja juu na kusawazisha goli hilo katika dakika ya 80 lililofungwa na Laurent Koscielny na 2 – 2 na hivyo kufanya mechi hiyo kutopata mshindi katika dakika 90 za kawaida.
Baadae mwamuzi wa mpambano huo Lee Probert aliongeza dakika nyingine 30 ambazo zilifanya Arsenal wajiongezee goli la tatu goli la ushindi katika dakika ya 108 lililofungwa na Aaron Ramsey.

wachezaji wa Arsenal wakishangilia goli la ramsey.

Hadi mpira unamalizika Arsenal wakawa wameifunga Hull City kwa jumla ya magoli 3 -2
Gunners ilishinda taji lake la mwisho mwaka 2005 katika
fainali za kombe la F.A ambapo iliwacharaza wapinzani wao wa
jadi Manchester United katika mechi iliochezewa katika uwanja wa
Cardiff,huku timu ya Hull City ikishiriki kwa mara ya kwanza katika
fainali ya kombe hilo.
Meneja Arsene Wenger ameshinda mataji saba muhimu katika miaka yake 18 kama mkufunzi wa timu ya Arsenal, ikiwemo mataji matatu ya ligi kuu ya uingereza pamoja na manne ya kombe la F.A.

Mashabiki wa timu zote mbili walikabidhiwa tiketi 25,000 kila mmoja huku tiketi nyengine 20,000 zikipewa watu waliojitolea katika mashirika ya hisani,vilabu na ligi za kaunti.
<<<<<BOFYA HAPA ULIKE PAGE YETU>>>>>
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro










Post a Comment
Post a Comment