
Afisa wa polisi akilinda mojawapo ya maeneo katika jiji la Nairobi ambalo usalama wake unatatiza.
Watu wanne, wakiwemo maafisa
wawili wa polisi, wameuawa jana usiku mjini Nairobi baada ya gari
walilolizuia kulipuka, lilipokuwa likielekea katika kituo cha polisi
katika eneo la Pangani, jijini Nairobi.
Bomu la pili lilipatikana katika gari hilo baada ya mlipuko huo na wataalamu wa mabomu waliliharibu.
Usalama umeimarishwa katika eneo hilo na polisi wanaendelea kufanya uchunguzi.
Bosco Mugendi ana kibanda cha kuuza vitu
vidogovidogo karibu na lango la kuingia kwenye kituo cha polisi cha
Pangani kulikotokea mlipuko huo.
Alunukuliwa akisema:"kile kilichonikuta katika kibanda changu ni nyama ya watu iliyonirukia halafu mimi nikatoroka na kutoka nje."
Mtaalamu wa maswala ya usalama jijini Nairobi, George Musamali, aliambia BBC kuwa maafisa wa polisi waliokuwa wakisindikiza gari kuelekea kituo hicho cha polisi walikuwa kwenye gari la washukiwa ambalo lililipuka baadaye.
Chanzo bbcswahili
<<<<<<BOFYA HAPA ULIKE PAGE YETU PLEASE>>>>>
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro








Post a Comment
Post a Comment