Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

Watu 25 walijeruhiwa vibaya katika shambulizi hilo lililotokea Jumatatu usiku
Polisi nchini kenya wanasema kuwa wamewakamata zaidi ya watu 200 kufuatia mashambulizi ya hapo jana Jijni nairobi ambapo takriban watu sita waliuawa.

Wengine 25 walijeruhiwa katika mashambulizi hayo matatu yaliotokea kwa wakati mmoja katika mtaa wa Eastleigh ambapo raia wengi wa kisomali wanaishi na kufanya kazi.

Polisi wanasema kuwa milipuko hiyo iliyotokea katika mikahawa miwili midogo huenda ilisababishwa na magurunedi pamoja na mabomu la kujitengezea.

Kumekuwa na mashambulizi kadhaa mjini Nairobi pamoja na mjini Mombasa katika miezi ya hivi karibuni ,ambapo polisi wanawalaumu waislamu wenye itikadi kali.
chanzo bbcswahili

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top