Tanzania Entertainment News,Politics News ,Celebrity Gossip and Live Updates
Home
»
SIASA
» -Watu wanne wanashikiliwa na Jeshi la Polisi wilayani Kibondo kwa kosa la kutaka kuvuruga mkutano wa Katibu Mkuu wa CHADEMA Dk Wilbrod Slaa
Jeshi
la Polisi wilayani Kibondo limewakamata watu wanne kwa kosa la kutaka
kuvuruga mkutano wa Katibu Mkuu wa CHADEMA Dk Wilbrod Slaa unaoendelea
muda huu katika kata ya Mabamba wilayani Kibondo
Mwandishi wa
Redio Kwizera Fm James Jovin amesema kuwa watu hao walikuwa na mabango
yenye maneno yanayoonesha kupinga uamuzi wa Kamati Kuu ya CHADEMA ya
kuwavua madaraka Zitto Kabwe na wenzake, lakini hata hivyo wameelekezwa
sehemu ya kukaa ili mabango yao yaweze kusomwa vizuri na Dk Slaa,
wamekaidi malelekezo hayo ambapo imebidi Dk Slaa aliagize jeshi la
Polisi kuwakamata watu hao kwani mkutano huo ni kwa mujibu wa sheria
Watu hao ambao majina yao hayakujilikana papo hapo wamepelekwa kituo
cha Polisi na Dk Slaa amemuagiza Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Kibondo
kufuatilia kesi hiyo kwa ukaribu
Source;JAMES JOVIN, REDIO KWIZERA
Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi
Post a Comment
Post a Comment