Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
                               
wachezaji wa liverpool wakishangilia baada ya kufunga goli mojawapo kwenye mchezo huu. 
Baada ya jana man city kumshushia kipigo Arsenal cha mbwa mwizi leo jioni ilikuwa siku nzuri kwa timu ya Liverpool pale walipo ishushia kipigo cha hatari sana huku luis suarez akitupia magoli mawili ktika mchezo huo uliochezwa kwenye uwanja wa white hart line .
Iliwachukua dakika kumi na nane pale mshambuliaji wao hatari raia wa urugay luis suarez alipoipatia goli la kwanza kweny mchezo huo na 84’ suarez akaifungia goli la nne, pia atika dakika ya 40 kiungo Henderson aliipatia bao la pili timu yake , dakika ya 75 beki wa kulia wa Liverpool alipokea pasi mulua kutoka kwa suarez na kutupia mpira nyavuni ,winga stering dakika ya 89 aliipatia Liverpool goli na kuhitimisha ushindi wa leo wa magoli matano kwa bila na Liverpool kuwa nyuma ya Arsenalkwa point 2 huku Liverpool wakiwa na 34  juu ya celsea na man city.
Ilikuwa ni siku nzuri sana kwa mshambuliaji wa timu hiyo luis suarez alipofunga magoli mawili na kutoa pasi mbili za magoli .
 
Kiungo wa tottenham  paulinho alionyeshwa kadi nyekundu baada ya kumchezea Luis suarez mchezo mbaya katika dakika ya 63 ya mchezo na timu yake kumaliz ikiwa pungufu ya mchezaji mmoja.

Mechi iliyotangulia kabla ya Liverpool Manchester united bada ya kupoteza mechi mbili mfululizo leo wamepata ushindi kwa kuifunga aston villa magoli 3 kwa bila.
Mshambuliji wao Welbeck katika dakika ya 15 na 18 aliipatia timu yake maoli mawili ya araka haraka na kuiweka Manchester kwenye nafasi nzuri ya kuhukua point tatu kwnye mechi ya leo.
Ilikuwa ni siku nzuri pale kiungo mkabaj wa timu hiyo Fletcher aliporejea kikosini baada ya kukaa nje kwa kipindi kirefu .
Iliwachukua dakika ya 52 kiungo wa timu hiyo cleverly alipotupia goli ta 3 na la mwisho kwenye mchezo huo uliochezwa kwenye uwanja wa villa park. swansea na norwich city zimetoka sare ya goli 1 kwa 1.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top