Hivi
karibuni hapa jiji mwanza mkazi mmoja wa Igoma Aliefahamika kwa jina
moja la Consolata amepigwa na mmewe na kung’atwa sikio na mtu anaedaiwa
kuwa ni hawara wa mumewe bi consolata amesema alikuwa akigombana na
mumewe ndipo hawara yake huyu alipokuja na kusema ngoja tukuonyeshe
maana hutujui ndipo alipong’atwa sikio na kuondolewa sikio zima
Mara baada ya kufanyiwa ukatili huo alienda kulipoti katika kituo cha polisi lakini kwa
madai yake ni kwamba watuhumiwa waliachiwa huru kwa kuwa walikuwa
wakijuana na baadhi ya askari waliokuwepo kituoni .Ndipo bi consolata
alipochukua hatua za kutafuta wasamalia wema kama waandishi ili waweze
kumsaidia aweze kupatiwa matibabu kwani ni mgeni jiji mwanza toka kigoma
na alikuja mwanza kwa ajili ya kumsalimu mumewe.
Baada ya
kuzungumza na waandishi alipelekwa kwenye taasisi ya kivulini ambao
mpaka sasa wanampatia huduma ya matibabu ukatili huu kiukweli ni aibu
kubwa kwa taifa letu
Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi
Post a Comment
Post a Comment