
Yingluck Shinawatra,waziri mkuu Thailand
Waziri Mkuu wa Thailand, Yingluck Shinawatra, amepona kung'olewa madarakani baada ya kushinda kura ya kutokuwa na imani naye.
Ameshinda kirahisi kwa kupata idadi kubwa ya kura alizohitaji kutoka baraza la chini la bunge la nchi hiyo, ambalo wajumbe wake wengi ni kutoka muungano wa chama chake.
Waandamanaji ambao walizingira majengo ya wizara kadha mjini Bangkok wamesema watasitisha kwa muda maandamano yao.
Wanasema lengo lao ni kuondoa mfumo mzima wa siasa kwa sababu wanafikiri mfumo huo umehodhiwa na kaka yake waziri mkuu Yingluck, Taksin Shinawatra ambaye anaishi uhamishoni.
---BBC
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro







Post a Comment
Post a Comment