Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini, Aziz Abood ambaye ndiye mmiliki wa Kituo cha Abood Media alipokuwa akifanya kazi marehemu Nyaisangah akimpa mkono wa pole mke wa marehemu, Leah Nyaisangah nyumbani kwake Kihonda Mtaa wa Viwandani mkoani Morogoro.

Mke wa marehemu, Leah Nyaisangah akiwa na simanzi baada ya kuondokewa na mumewe.

Baadhi ya waombolezaji wakiwa msibani kwa marehemu Julius Nyaisangah eneo la Kihonda Mtaa wa Viwandani mkoani Morogoro.

MAREHEMU Julius Nyaisangah 'Uncle J' amefariki dunia leo asubuhi baada ya kuugua kwa muda mrefu. Akizungumza na Mtandao huu, Mke wa marehemu, Leah Nyaisangah amesema kuwa mumewe alilkuwa akisumbuliwa na magonjwa ya sukari na shinikizo la damu kwa muda mrefu na amefariki leo asubuhi. Marehemu Nyaisangah mpaka mauti yanamfika alikuwa Meneja Mkuu wa Abood Media iliyopo mkoani Morogoro. Marehemu ameacha mke na watoto watatu ambao ni Samwel, Noela na Beatrice. Mwili wa marehemu unatarajiwa kusafirishwa kwa mazishi yatakayofanyika nyumbani kwao Tarime.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top