Emma Roberts ni binti mwanafunzi aliyekumbwa na mkasa wa kufukuzwa shule kutokana na ujauzito alioupata baada ya kubakwa. Kupitia kipindi cha Wanawake Live kinachorushwa na East Africa Television kila Jumanne saa tatu usiku, binti Emma anaelezea tamaa yake ya kufanya mtihani mwezi Novemba, kwa kuwa anaamini kuwa elimu itamsaidia yeye na mwanaye ambaye atalelewa bila kuwa na baba. Kitendo cha kufukuzwa shule kwa tukio kama hili kumemuathiri kwa kiasi kikubwa, na sasa ana hofu ya kutimia kwa malengo yake hapo baadae.
Kumnyima fursa hiyo ya kuendeleza elimu yake ni kutengeneza taifa lenye wanawake wasio elimu na masikini. Kitendo kilichomkuta Emma, kinaweza kuwakuta wasichana wengi nchini Tanzania. Kuna wale waliojitokeza hadharani, lakini vipi kuhusu wale walioamua kukaa kimya?
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro








Post a Comment
Post a Comment