Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Kwa mtazamo wangu ndoa ni muhimu pamoja na ukweli kuwa baadhi ya ndoa zina matatizo, lakini bado zinadumu. Msingi wa ndoa nyingi kuwa mbaya ni kwa sababu wengi wanaanza vibaya. Msichana unamtongoza saa 2:15 lakini ikifika saa 2:45 tayari mko nyumba ya wageni. Nilikuwa nazungumza na jamaa mmoja, akaniambia siku hizi kupata chumba kwenye nyumba hizo ni ngumu zaidi kuliko kumpata mwanamke. Lakini kwanini wanawake wanajirahisi? Ni kwasababu wengi wako kimaslahi zaidi. Wanategemea kuvuna, anajua ukienda naye, siyo rahisi usimpe hata nauli, soda, fedha nk. Wapo pia wanaume wenye tabia hizi, anakuwa na mwanamke kwa sababu ya kutegemea kuhongwa chochote kitu. Yaani kuna wanaume wengine, bajeti ya nyumbani ni mke mwenye kufanya kila kitu. Wengine wanakuwa wepesi wa kuingia kwenye ngono, kwa sababu ya kuangalia au kufuatilia simulizi za mambo ya ngono. Hata hivyo lililo la msingi katika maisha ni kuwa na muda wa kuzungumza ili kuondoa tofauti, kila mtu anapaswa kuwajibika. Ni makosa makubwa kwa mfano mwanaume au mwanamke kujinunulia nguo za ndani. Mwambie mwenzi wako, kuanzia leo suala la nguo hizi za ndani ni lake, ikiwezekana mpe kipande cha gazeti asome. Hata kama mtu ataamua kujinunulia, bado mwenzi wake ndiye hasa mwenye kupaswa kumnunulia. Hii ni mojawapo ya faida ya kuoa au kuolewa, kwamba angalau unakuwa na mtu ambaye anawajibika juu ya mwili wako. Jambo jingine la msingi sana katika ndoa, ni makosa makubwa kunyimana. Ninalizungumza hili mara nyingi kwa sababu ndilo linalosababisha watu wengi kwenda nje ya ndoa. Maana kuna wengine ukimlazimisha sana anasema kwa hasira �haya njoo, au hutaki, nataka kuwahi kuandaa watoto bwana�. Ukweli ukiambiwa hivi, shauku yote inakwisha. Mapenzi yanahitaji mwenzi wako pia aonyeshe kuhitaji, si kufanya kama hivi. Iwe ni mtu maarufu, iwe ni mtu mwenye fedha, iwe ni mtu masikini au mtu wa hali yoyote, bado kuna faida kubwa ya kuoana. Mnapokuwa kwenye ndoa, iko heshima kutoka kwa jamii, pia ndoa inakupa hadhi ya aina yake mbele ya Mungu.

Hakuna aliye kamili katika dunia hii, hata Mungu anakusamehe kwa njia zako na matendo yako, si kweli kwamba wewe ni msafi sana hadi leo bado uko hai, bali Mungu ni mwenye huruma anakusamehe. Aidha unapaswa kufahamu kuwa kuna faida za kuoa mapema. Ndoa tamu bwana asikwambie mtu tena ni raha uipate ndoa ukiwa kijana, nyumba ujenge ukiwa kijana, gari ununue ukiwa kijana, siyo hadi unakuwa babu. Faida ni kujenga maisha mapema, kujipanga vizuri na kujenga familia. Ni furaha unapokuwa na watoto ambao ni kama wadogo zako. Kuzaa ujana ni raha zaidi, kuliko ukizaa ukiwa na zaidi ya miaka 35. Pia usiogope kuoa mapema kwamba eti utapitwa na mambo ya ujana si kweli, mambo ya kujinafasi bado yapo, yalikuwepo na yataendelea kuwepo na yanakuwa ni ya kiutu uzima zaidi, ni ya staha na heshima mbele, fujo fujo hakuna. Pia kuna tafiti za kisayansi zinaonyesha watu wanaopata watoto wakiwa na zaidi ya umri wa miaka 35, wanapata watoto wenye akili ndogo. Wenye hoja za kutokuwa na mpango kabisa wa kuoa, wana matatizo ya kisaikolojia na wanapaswa kuachana na fikra hizo mbaya kwamba kuoana ni kubaya. Ukizoea sana kuishi kisela au kubadili wanaume au wanawake kama nguo, mwishowe unakuwa huwezi tena kutulia, na ndiyo hao ambao baadhi yao wamekuwa wakiona hakuna haja tena ya kuoana. Kuna wanaoogopa kuoa au kuolewa wakiamini ni jela fulani hivi, kumbe hilo si la kweli. Ukweli ni kwamba ukiwa kwenye uhusiano na mkaelewana vizuri, mafanikio huwa makubwa. Katika maisha pia kuna suala la nyota, kwamba wapo watu ambao ukiwa nao ni kama kujitia mikosi, kuna mwingine ukiwa naye tu, unashangaa mambo yanakwenda safi, ni suala la kutafakari kwa makini suala la kuwa na mwenza ambaye ni wa kudumu na ambaye anatambulika kisheria na mbele ya Mungu.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top