Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This


 
YANGA, ambayo imemrejesha kikosini mchezaji mwenye mapenzi makubwa na timu hiyo, Mrisho Ngassa, imepeleka haraka haraka mkataba wake kwenye Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), lakini mabosi hao wa soka nchini wakaupiga chini.
Kwa mujibu wa TFF usajili umeshaanza na mikataba ya wachezaji itaanza kupokelewa katikati ya mwezi huu kabla ya kuanza kupitiwa na kamati husika kuangalia uhalali wake mwishoni mwa Julai.
Yanga, ambao msimu huu hawasajili wachezaji wengi iliwasilisha mkataba wa Ngassa wiki iliyopita, lakini watendaji wa TFF wakagoma kupokea kwa madai kwamba bado muda wake haujafika.
“Mikataba yote itaanza kupokewa Julai 15, kwa hiyo tumewaambia Yanga kuwa wasubiri kwani muda wa kuleta mikataba bado,” kilisema chanzo kutoka TFF.
Mabingwa hao wa Tanzania ambao walimsainisha Ngassa mkataba wa miaka miwili walikuwa wakishinikiza mkataba huo ubaki kwa shirikisho hilo ili kuepuka fitina zinazoweza kufanywa na Simba ambao wamekuwa wakidai kwamba wana mkataba na Ngassa.
Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh ambaye inadaiwa ndiye aliyepeleka mkataba huo aligoma kutamka lolote alipoulizwa. Yanga ipo kwenye mikoa ya Kanda ya Ziwa kwa ziara ya mechi za kirafiki kujiandaa na msimu mpya ikiwa imeambatana na Ngassa.
Kwa mujibu wa kanuni ya 35 ya Ligi Kuu Bara inayohusu kipindi cha usajili kifungu cha “(2) Klabu zinawajibika kutumia mikataba iliyotayarishwa na Shirikisho kuhamisha/kuazima na kusajili wachezaji wake, mikataba mingine yote haitatambulika.
“(3) Kutangaza wachezaji ambao klabu inasitisha mikataba yao, uhamisho na usajili wa wachezaji utafanywa na walimu wa klabu katika kipindi kitakachotangazwa na TFF.”
                     mwanaspoti

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top