Jo’burg, Afrika Kusini.
Tangu kuanza kuumwa kwa Nelson Mandela, watu mbalimbali wamekuwa
wakifuatilia mambo mbalimbali yanayohusu maisha yake, mambo yote
aliyoyafanya.
Wapo wengine wanaofuatilia kwa karibu hali yake kiafya, ingawa hofu imekuwa maisha nchini humo baada ya kifo chake.
Hata hivyo, miongoni mwa vivutio vikubwa ni Daraja la Nelson Mandela jijini Johannesburg.
Hili ni daraja kubwa ambalo lilikamilika kujengwa
mwaka 2003, lakini kwa sasa limegeuka kivutio kwa maelfu ya wageni na
wenyeji wanaolitembelea, kupiga picha za ukumbusho.
Likiwa na urefu wa mita 248, daraja hilo linapamba anga la Johannesburg kwa rangi za upinde wa mvua hasa nyakati za usiku.
Kwa ufupi, daraja hilo linatumika juu ya njia ya
reli inayounganisha vitongoji vya Newtown na Braamfontein, jirani na
eneo maarufu la kibiashara lililogharimu Rand 38-milioni.
Wabunifu wake walitaka kuongeza kitu katika uzuri
wa jiji hilo la kisasa, kupendezesha eneo la katikati ya jiji hili kwa
kulipa sura ya kuvutia.
Lengo lake likiwa ni kuunganisha kitongoji
kinachokua cha Newtown na eneo la kibiashara la Braamfontein, pia
kuwezesha kuyafikia maeneo hayo kwa urahisi wakati wote.
Ujenzi wake mwanzoni ulionekana kuwa changamoto
kubwa kwa timu ya wabunifu na wahandisi wake kupita eneo ambako njia 42
za reli zinapishana bila kuingilia usafiri au kusababisha misongamano ya
magari.
Kwa jumla, daraja hilo la Mandela ambalo ni
ubunifu wa Kampuni ya Dissing & Weitling, ndilo kubwa la waya Kusini
mwa Afrika.
Liliandaliwa maalumu kuwa jepesi, likichanganya
vyuma na vifaa vingine vya kuliwezesha kuwa jepesi kwa kadri
inavyowezekana, lakini lenye nguvu ya kutosha.
Kulingana na mtandao wa Engineering News, kiasi
cha mita za mraba 4,000 za zege, tani 1,000 za vyuma zilitumika kwenye
ujenzi wake na tani 500 zaidi ya vyuma maalumu vya kushikilia msingi
wake.
Daraja hilo si heshima pekee kwa Afrika Kusini na kiongozi wake
wa kwanza wa kuchaguliwa, Nelson Mandela, bali ujenzi na muundo wake ni
utambulisho wa jinsi kiongozi huyo alivyobaki kiunganishi cha raia
waliotengwa na ubaguzi wa rangi.
Wengi wanalitumia daraja hilo kama njia ya kuliona
vyema anga la jiji hili. Kwa madereva wengi, wanaendesha magari juu
yake au hupenda kulitazama wakiendesha kwa mwendo taratibu, kutembea juu
kupitia njia ya waendao kwa miguu. Pia, kuna njia ya waendesha baiskeli
ili kuhakikisha kwamba wako salama wakati wanapovuka eneo hilo la jiji
lenye shughuli nyingi.
Daraja hilo lina njia rahisi ya kuliona jiji bila
malipo, ingawa wageni wanashauriwa kufurahia mandhari yake kwa mguu hasa
wakati wa shughuli nyingi jijini humo.
mtanzania
mtanzania
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
Post a Comment
Post a Comment