Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Minister_Mr_Bernard_K_Membe
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe alisema Serikali imetambua umuhimu wa Watanzania kuruhusiwa kuwa na uraia wa nchi mbili. Hatua hii imepelea Serikali kupendekeza kwenye Tume ya Mabadiliko ya Katiba ili suala hilo lifikiriwe kuingizwa kwenye Katiba Mpya ambayo mchakao wa kuiandaa unaendelea.
Waziri Membe aliyasema hayo alipokuwa akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara yake mwaka 2013/14 kwenye mkutano wa kumi na moja wa Bunge la Bajeti mjini Dodoma.

Alisema suala la uraia wa nchi mbili limekuwa likiwatatiza Watanzania walioko nje ya nchi kwa mambo mengi, ikiwamo kujihusisha kwenye shughuli mbalimbali za maendeleo nchi wanazoishi.
Waziri Membe alisema Wizara yake katika maoni yake kwa Tume ya Katiba, ililipa suala la uraia wan chi mbili kipaumbele kwa kuamini kuwa hatua hivyo itwawezesha Watanzania waliopo nje kuchangia kwa kiwango kikubwa maendeleo ya nchi yetu kama inavyofanyika katika nchi zingine ambazo sheria hiyo inatumika.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top