Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This



            Focas Malengo Afisa Mnadhimu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe
                        .....................................................................................................................

Watu wanaosadikika kuwa ni majambazi wakiwa na silaha mbali mbali zikiwemo wa moto wamevamia kituo cha Mafuta cha Oreyx kilichopo mjini Mkambako mkoa wa Njombe na kufanya mauwaji ya kinyama kwa walinzi wawili na kujeruhi mmoja kabla ya kupora kiasi cha zaidi ya Tsh milioni 7



Mashuhuda wa tukio hilo wameueleza mtandao huu kuwa tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia jana .

Mashuhuda hao walisema kuwa majambazi hao wawili wakiwa na usafiri wa piki piki ambapo walifika katika kituo hicho kwa ajili ya kununua mafuta ya Tsh 5000 na wakati wakiendelea kuhudumiwa ghafla walianza kuwashambulia walinzi kwa risasi na kuwaua walinzi wawili na kumjeruhi meneja wa kituo hicho.

Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Focas Malenge amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataja waliouwawa kuwa ni Jonas Mpogole na Chesco Sanga ambao ni walinzi wa kampuni ya ulinzi ya Makambako .

Mbali ya kuwaua walinzi hao wawili pia majambazi hayo yalimjeruhi kwa risasi meneja wa kituo hicho Jonas Msenyi na kupora fedha zaidi ya Tsh milioni 7

Alisema kuwa jeshi la polisi linaendelea na msako wa kuwasaka majambazi hayo ikiwa ni pamoja na kuwaomba wananchi kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo la polisi

CHANZO: MATUKIODAIMA BLOG

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top