Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Khadija Omar Kopa akiwa na mumewe Jaffari Ally enzi za uhai wake.
Taarifa nilizozipata mapema leo alfajiri zinasema kwamba Mume wa Malkia wa Mipasho,  Bi. Khadija Kopa, aitwaye Jaffari Ally amefariki dunia usiku wa kuamkia leo mida ya saa 9 usiku, Katibu wa Bendi ya TOT Gasper Tumaini amethibitisha juu ya msiba huo.

Taarifa za awali zinasema kwamba chanzo cha kifo chake ni ugonjwa wa Maralia, ambapo siku ya Jumatatu marehemu Ally alipelekwa Hospitali ya Lugaro kwa ajili ya kupata matibabu.


Taarifa zaidi zinasema kwamba marehemu alipata nafuu na kurudi nyumbani kwao Bagamoyo, hali ambayo ilimpelekea Khadija Kopa kusafiri kikazi, na inasemekana mpaka umauti unamkuta Jaffari Mkewe Khadija Kopa alikuwa yupo kikazi mikoani kwa ajili ya shughuli zake za kimuziki.

Pole sana Bi. Khadija Kopa kwa kumpoteza Mumeo Mpendwa, Mungu akutie nguvu katika kipindi hiki kigumu. 

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top