Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Unalizungumziaje suala la nguo fupi kwenye filamu?
Moja ya mambo yanayojadiliwa sana na vyombo vya habari kwa sasa, ni suala la kina dada wa bongo movies kupenda kuvaa nguo fupi sana wanapokuwa wanaigiza filamu zetu hizi.

 Ikizingatiwa ni karibuni tu, suala hili lilijadiliwa mpaka bungeni na pia siku chache zilizopita mwigizaji maarufu nchini Simon Mwakifamba aliongea na chombo kimoja cha televisheni na kusema kuwa wadada hawa lengo lao ni kuonesha miili yao kwa lengo la kujiuza, sisi tukiwa kama tovuti rasmi ya filamu Tanzania tungependa kupata maoni yako wewe mdau na mpenzi wa tasnia yetu hii, Je, wewe unalichukuliaje suala hili? Ni kweli haya madai yana maana na inabidi yafanyiwe kazi au wanafanya hivyo kama sehemu ya sanaa? Tupia maoni yako hapo chini mdau.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top