Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Mwigizaji Halima Yahya “Davina” amekuwa sio mchoyo wa shukrani baada ya kufunguka yake ya moyoni kwa kile ambacho migizaji mwenzake, Steve Nyerere alichokifanya hapo jana kwenye uzinduzi wa kundi lao jipya la KAONE. Nahivi ndivyo alivyofunguka;

"Dah kiukwel napenda kuchukua nafasi  hii kumshukuru huyu mtu (SteveNyerere) kwa support kubwa aliyotupa jana katika uzinduzi wa kundi la #KAONESANAAGROUP ,ahsante sana jamani yaan kiukweli mnyonge mnyongen haki yake mpeni na sisi Watanzania tuna kawaida ya kumsifia mtu akiwa hayupo Dunian lakini  Stevenyerere una moyo wa pekee sana kiukwel  kama kuna ambae namkwaza anisamehe lakini  huyu baba anajitoa sana katika mambo ya wenzie sawa ana vimatatzo kidogo vya  hasira sana wahehe tunasema  anakidadaa na anaweza kasirika na akanuna lakini  sio mtu wa kuweka vitu moyoni na mifano ninayo any way nusiongee mengi ila Mungu akubariki kaka kwa moyo wako huo na akuxidishie zaid na zaid inshaallah. .”.
Davina alimaliza

Kundi la KAONE SANAA GROUP  ambalo linaundwa na wasanii wa kundi la zamani la kaole ilizindulitukiwa  hapo jana  pale Dar Live na mgeni rasmi alikuwa  Mh January Makamba.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top