Mwigizaji Halima Yahya “Davina” amekuwa sio mchoyo wa shukrani baada ya kufunguka yake ya moyoni kwa kile ambacho migizaji mwenzake, Steve Nyerere alichokifanya hapo jana kwenye uzinduzi wa kundi lao jipya la KAONE. Nahivi ndivyo alivyofunguka;
"Dah kiukwel napenda kuchukua nafasi hii kumshukuru huyu mtu (SteveNyerere) kwa support kubwa aliyotupa jana katika uzinduzi wa kundi la #KAONESANAAGROUP ,ahsante sana jamani yaan kiukweli mnyonge mnyongen haki yake mpeni na sisi Watanzania tuna kawaida ya kumsifia mtu akiwa hayupo Dunian lakini Stevenyerere una moyo wa pekee sana kiukwel kama kuna ambae namkwaza anisamehe lakini huyu baba anajitoa sana katika mambo ya wenzie sawa ana vimatatzo kidogo vya hasira sana wahehe tunasema anakidadaa na anaweza kasirika na akanuna lakini sio mtu wa kuweka vitu moyoni na mifano ninayo any way nusiongee mengi ila Mungu akubariki kaka kwa moyo wako huo na akuxidishie zaid na zaid inshaallah. .”.
Davina alimaliza
Kundi la KAONE SANAA GROUP ambalo linaundwa na wasanii wa kundi la zamani la kaole ilizindulitukiwa hapo jana pale Dar Live na mgeni rasmi alikuwa Mh January Makamba.
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro






Post a Comment
Post a Comment