Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This
Oscar Pistorius
Mwanariadha wa Afrika Kusini asiye na miguu yote miwili Oscar Pistorius ameathirika vibaya kutokana na ulemavu wake, daktari wa michezo ameiambia mahakama inayosikiliza kesi ya mauaji inayomkabili mwanariadha huyo.

Wayne Derman ameiambia mahakama mjini Pretoria kuwa bingwa huyo wa olimpiki ameathirika vibaya "kutokana na msongo wa mawazo na hofu".
Bwana Pistorius anasema alimuua kwa kumpiga risasi rafiki yake wa kike Reeva Steenkamp baada ya kumdhania ni mwizi aliyeingia ndani ya nyumba yao mwaka jana.

Upande wa mashitaka unasema kuwa Pistorius alimuua kwa makusudi Bi Steenkamp baada ya kuzozana.
Suala linaloangaliwa ni akili ya Pistorius wakati akifyatua risasi dhidi ya Reeva.
>>>>>bbcswahili 

kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA
 

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top