Mwanamke
mweye umri wa miaka 29 aishie Washington,Marekani ameripotiwa kuzama
katika bwawa kubwa la kuvulia samaki wakati akijaribu kumuokoa mbwa wake
aliyetaka kuzama.
Mwanamke
huyo aliyetajwa kwa jina la Sabra Crafton, mkazi wa Cashmere,
Washington alikutwa na tukio hilo wakati akiwa na rafiki yake wa kiume
kando ya bwawa la kuvulia samaki.
Rafiki
yake huyo wa kiume alimuambia mkuu wa kituo cha polisi cha Chelan kuwa
walikuwa wanamrushia mbwa huyo vitu majini na yeye anavifuata kama
mchezo lakini baadaye mbwa huyo alionekana kutaka kuzama na ndipo Sabra
Crafton akaamua kuingia kumuokoa.
Hata hivyo hali ilikuwa mbaya kwa kuwa Mwanamke huyo alizidiwa na kuzama yeye na mbwa wake aliweza kutoka.
Afisa
wa polisi wa Chelan alieleza kuwa baada ya kupewa taarifa walifika
katika eneo la tukio na waliweza kumpata na kumtoa kwenye maji mwanamke
huyo na kumpa huduma ya kwanza kwa dakika 30 kabla hawajamkimbiza
hospitalini.
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro






Post a Comment
Post a Comment