Balozi wa Libya nchini Tanzania amejiua kwa kujipiga risasi kichwani.
Mwandishi wa BBC mjini Dar es Salaam , John
Solombi anasema kuwa balozi huyo kwa jina Ismail Nwairat, alijipiga
risasi Jumanne usiku na kufariki akiwa anapokea matibabu hospitalini.Msemaji wa serikali ya Tanzania Arthur Mwambene amethibitisha taarifa hiyo kuwa balozi huyo alijiua ndani ya makao ya ubalozi wa Libya mjini Dar es Salaam Jumanne usiku.
Uchunguzi unafanyika kubaini sababu ya kujiua kwa balozi hiyo.
kama huja like ukurasa wetu wa facebook fanya hivi sasa ili habari ziwe zinakuijia punde tu zinapoweka kwenye mtandao huu BONYEZA HAPA
Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro






Post a Comment
Post a Comment