Share this PostPin ThisShare on TumblrShare on Google PlusEmail This

 
Mkurugenzi wa lebo ya Watanashati Entertainment Ustaadh Juma na Musoma ameendelea kushutumiwa na kulaumiwa baada ya kusambaza video na picha zinazomuonesha msanii PNC amempigia magoti kuomba msamaha baada ya kutangaza kutoka katika kundi hilo.

Msanii wa Mwanza Hamis Ramadhan Baba Hbaba amemjia juu Ustaadh Juma akidai amemdhalilisha msanii mwenzao wa Mwanza kitendo ambacho hajakipenda.

Hbaba ni muendelezo wa wasanii na wadau mbalimbali wa muziki kuendelea kumshutumu Ustaadh Juma kwa kitendo hicho.

Tayari Meneja wa TMK Wanaume Said Fella,mkurugenzi wa Visual lab Adam Juma,msanii wa vichekesho Kitale,Isabela Mpanda na wasanii wengine kadhaa wameonesha kuchukizwa na kitendo hicho cha Ustaadh Juma na Musoma.

Je, Una Habari,Picha,Tangazo,Makala,

Hifadhi blog hii kwenye simu yako ili upate habari zote kwa urahisi zaidi

Facebook Blogger Plugin by Kibonajoro
http://www.facebook.com/kibonajoro

Post a Comment

 
Top